Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?

Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?

 Ndiyo, mara mingi Mashahidi wa Yehova wanasaidiaka wale wenye wanafikiwa na misiba. Tunasaidiaka Mashahidi wenzetu na wale wenye hawako Mashahidi, kulingana na maagizo yenye kupatikana mu Wagalatia 6:10: “Tutendee watu wote mambo ya muzuri, lakini zaidi sana wale wenye kuwa wa jamaa yetu katika imani.” Tunajikazaka pia kusaidia kihisia na kiroho wale wale wenye walifikiwa na misiba.​—2 Wakorinto 1:3, 4.

Mambo Yenye Tunafanyaka

 Kisha musiba kutokea, wazee wa makutaniko yenye kuwa mu eneo yenye ilipatwa na musiba, wanajikazaka kuongea na ndugu na dada ili kujua kama wako salama na ili kujua mambo yenye wako nayo lazima. Kisha wale wazee wanatumia biro ya tawi ripoti ya uchunguzi wao na wanafasiria mambo yenye walifanya juu ya kusaidia wale wenye walifikiwa na musiba.

 Kama ile makutaniko yenye kuwa mu ile eneo haina uwezo wa kusaidia wale wote wenye walifikiwa na musiba, Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova inafanya mipango ili kutoa musaada wenye unahitajiwa. Ni vile Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa nafanya ili kuhangaikia Wakristo wenzao wakati wa njala. (1 Wakorinto 16:1-4) Biro ya tawi yenye inasimamia ile eneo inaweka Halmashauri za Kutoa Misaada juu ya kusimamia kazi ya kusaidia wale wenye wanafikiwa na misiba. Mashahidi wa maeneo ingine wanatoa wakati wao na mali yao ili kusaidia​—Mezali 17:17.

Makuta

 Njia moya ya kutumia makuta ao michango yenye inatumwaka ku biro za tawi za Mashahidi wa Yehova ni kusaidia wale wenye walipatwa na misiba. (Matendo 11:27-30; 2 Wakorinto 8:13-15) Vile ile kazi inafanywa na watu wenye kujitolea, makuta yenye inatolewa inatumiwa juu ya kusaidia wale wenye walipatwa na misiba, hapana juu ya kulipa wale wenye kujitolea kufanya ile kazi. Tunatumiaka michango yote kwa uangalifu.​—2 Wakorinto 8:20.