Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

GEORGIY PORCHULYAN | HABARI JUU YA MAISHA YAKE

“Kumupenda Yehova Kulinisaidia Maisha Yangu Yote”

“Kumupenda Yehova Kulinisaidia Maisha Yangu Yote”

Nilikuwa tu na miaka 23 wakati nilitumwa mu kambi ya kazi ya nguvu mu Siberia, mu eneo ya Magadan. Ile wakati, kulikuwa kumepita mwaka moya tu tangu nikuwe Shahidi wa Yehova mwenye kubatizwa. Nilikuwa natenda bila kufikiri na sikukuwa na uzoefu. Kwa hiyo, siku moya wakati nilizungumuza na mufungwa mwenzangu kuhusu imani yangu, kulibakiaka kidogo tu tupigane.

 Sasa, nini njo ilinichochea niache kuwa Mukomunisti na kujiunga na kikundi ya dini yenye watu wengi waliona kuwa ilikuwa adui ya Serikali? Na namna gani kumupenda Yehova na mazoezi yenye alinipatia vilinisaidia nifanye utu wangu ukuwe muzuri zaidi miaka yote yenye nilifanya mu kambi ya kazi ya nguvu na pia mu uhamisho?

Nilikuwa natafuta Haki na Amani ya Akili

 Nilizaliwa mu 1930, mu Tabani, kijiji maskini yenye kuwa kaskazini ya Moldova. Wazazi wangu walitumika nguvu sana mu ferme juu ya kutulisha siye watoto sita. Hatukukuwa na vitu mingi vya kimwili. Mama yangu alikuwa mu Kanisa ya Ortodoksi ya Urusi, na baba yangu alikuwa Katoliki. Mara mingi walikuwa wanabishana juu ya mambo ya mubaya yenye mapadiri walikuwa wanafanya.

 Nilipata diplome wakati nilikuwa na miaka 18, kisha nilijiunga na kikundi ya vijana wenye walikuwa nafundisha Ukomunisti. Ile kikundi ilikuwa inaitwa Komsomol. Kusudi yao ilikuwa kufundisha vijana juu wajiunge na kikundi ya Wakomunisti. Kisha wakati kidogo niliwekwa kuwa muandishi wa ile kikundi mu kijiji yetu. Kule, nilifurahia kujifunza kama watu wote ni ndugu na dada, wako sawasawa, na wanapaswa kutendewa bila ubaguzi, lakini nilivunjika moyo wakati niliona ukosefu wa haki na rushwa ao kata midomo vyenye vilikuwa mule.

 Vile nilikuwa mu ile kikundi ya Komsomol, nilipaswa tu kufuata maagizo ya serikali ya Muungano wa Sovieti,  a yenye ilisema kama iliomba kufunga makanisa yote na kuvunja vikundi mbalimbali vya kidini. Mu kijiji yetu kulikuwa Mashahidi fulani wa Yehova. Nilijua kama walikuwa wanyoofu na wenye kufanya amani, niliona kama walikuwa watu wenye kuwa na musimamo wa nguvu mu mambo ya dini. Lakini, sikujua kama kisha wakati fulani mumoya kati yao angenijibia maulizo yangu.

 Mujomba yangu Dimitriy, mwenye alikuwa naishi mu kijiji yetu alikuwa Shahidi wa Yehova. Siku moya, mu Mwezi wa 5, 1952, aliniuliza hivi: “Georgiy, unapanga kufanya nini mu maisha yako?” Ni yeye tu njo aliniulizaka ile ulizo na ilionyesha kama ananihangaikia. Kusema kweli, nilikuwa na maulizo mingi yenye haikukuwa na majibu. Kwa mufano, mara mingi nilikuwa najiuliza hivi: ‘Kama Mungu iko, juu ya nini anaacha watu wateseke sana?’ Mu siku munane zenye zilifuata, Dimitriy alitumia Biblia ili kujibia maulizo yangu. Wakati fulani tulikuwa nazungumuza juu ya Mungu mupaka saa kenda (3:00) ya asubui!

Wakati fulani Georgiy na Dimitriy walikuwa najifunza Biblia mupaka usiku sana

 Kisha ile mazungumuzo, niliamua kujifunza Biblia kwa uangalifu sana. Nilianza kutambua kama nilikuwa na Baba wa mbinguni mwenye alinipenda sana. (Zaburi 27:10) Hata kama sikujua mambo mingi mu Biblia, kumupenda Yehova kulinichochea niazimie kufanya jambo fulani. Niliachana na ile kikundi ya Wakomunisti hata kama musimamizi wetu aliniogopesha. Miezi ine tu kisha kujifunza Biblia, nilijitoa kwa Yehova na kubatizwa mu Mwezi wa 9, 1952.

Kumupenda Yehova Kulifanya Nipate Majaribu

 Ile wakati, kazi ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa imekatazwa. Lakini, nilipenda kumuonyesha Yehova kupitia matendo yangu kama namupenda. Kwa hiyo nilianza kusaidia mu kazi ya kupelekea Mashahidi wenzangu, wenye walikuwa wanaishi mu vijiji vingine, vichapo vyenye vinategemea Biblia. Kufanya vile ilikuwa hatari juu ilikuwa mwepesi sana kwa wakaaji wa mu kijiji kushitaki mugeni kama wanakuwa na mashaka juu yake. Kwa kweli, hata Mashahidi fulani walikuwa na mashaka juu yangu, walikuwa naogopa kama pengine nilikuwa mumoya kati ya polisi wenye walikuwa najifanya waonekane sawa vile ni Mashahidi wa Yehova. Lakini, kisha wakati mufupi walifikia kutambua kama sikukuwa mupelelezi. Miezi mbili tu kisha kubatizwa, nilifungwa na kushitakiwa kama nilikuwa napatia watu vichapo vyenye serikali ilikataza.

 Wakati nilikuwa mu ile kifungo ya muda yenye ilifanya karibu mwaka moya, polisi waliniuliza maulizo mingi juu nivunje ushikamanifu wangu. Lakini nilikuwa nilishamupenda Yehova sana. Ku mwisho, nilienda kusikilizwa ku tribinali yenye ilikuwa mu muji wa Odessa, mu Ukraine. Ile wakati wazazi wangu na ndugu na dada zangu wenye hawakukuwa Mashahidi wa Yehova, waliitwa pia kule ku tribinali.

 Tribinali ilinihukumu kwa kusema kama niliingia mu sekte ya hatari. Wenye mamlaka walipenda wazazi wangu na ndugu na dada zangu waamini kama nilipata wazimu. Wazazi wangu waliogopa. Walilia na kuniomba niachane na Mashahidi wa Yehova. Lakini nilibakia kimya. Nilimuambia mama yangu hivi: “Usiogope. Sikujidanganya. Nimepata jambo yenye nilikuwaka natafuta maisha yangu yote, na sitaiacha hata kidogo.” (Mezali 23:23) Sikujua mambo mingi mu Biblia, lakini mambo yenye nilijua juu ya Yehova ilinisaidia nishikamane naye kabisa. Kisha miaka sita hivi, wazazi wangu walianza kufurahia mambo yenye niliamini na walifikia pia kuwa Mashahidi wa Yehova.

Tribinali ilimushitaki Georgiy mbele ya wazazi wake, kwa kusema kama alifanya kosa ya kuiingia mu sekte yenye kuwa hatari

 Nilihukumiwa kifungo ya miaka 15 ya kazi ya nguvu. Kisha nilipelekwa mu eneo ya Kolyma kupitia train. Mu ile eneo, mulikuwa kambi mingi za kazi ya nguvu. Juu ya kunyenyekeza kabisa wafungwa, walinzi na polisi walikuwa natupiga na kutuima chakula. Ku mwanzo, nilikuwa najiuliza kama kweli nitaendelea kuishi.

Mungu Alinihangaikia kwa Upendo na Kunizoeza

 Wakati fulani kisha tu kufika, Mashahidi wa Yehova 34 wenye walikuwa pia wafungwa mu ile kambi, waliniuliza hivi kwa busara: “Kuko Yonadabu yeyote mu kikundi yenu?” Palepale nikajua kama walikuwa Mashahidi wa Yehova wenzangu juu ni wao tu njo walikuwa natumia ile neno ya mu Biblia! Wale ndugu wenye kuwa na uzoefu walinisaidia nijue kutumikisha muzuri kanuni za Biblia mu hali zenye kuwa nguvu. Zaidi ya ile, walinisaidia nionyeshe sifa mbalimbali za kiroho, sawa vile utambuzi.

 Mu ile kambi nilikuwa natembeza mashini. Siku moya, mufanyakazi mwenzangu mwenye kuitwa Matphey alikuwa najisifu kama alijua majina 50 ya watakatifu. Wakati nilisema mubaya juu ya wale watakatifu, Matphey alijaribu kunipiga ngumi, lakini nikakimbia. Kisha, nilikasirika wakati niliona ndugu zangu wako nanicheka. Niliwauliza hivi: “Juu ya nini muko nanicheka? Nilikuwa nataka kuhubiri!” Walinikumbusha kwa upole kama kusudi yetu ni kutangaza habari njema, hapana kukwaza watu. (1 Petro 3:15) Hata kama Matphey hakukuwa anakubaliana na serikali, alikuwa nafurahia sana kuona namna Mashahidi wa Yehova wakuwa naheshimia walinzi na watu wenye mamlaka. Ku mwisho, alianza kupendezwa na mafundisho ya Biblia. Nitaendelea kumbuka usiku wenye alibatizwaka kwa siri mu maji ya baridi.

 Wakati kidogo kisha kufika mu kambi, miye na ndugu wawili tulialikwa ili kusoma masomo fulani ya politike. Ku mwanzo, tulikuwa nakatala kuhuzuria mikutano kwa ajili ya ile masomo. Tuliwaza kama ikiwa tunafanya vile tutavunja musimamo wetu wa Kikristo wa kutounga mukono upande wowote. (Yohana 17:16) Juu tulikatala kufanya vile, tulifungwa mu chumba kwenye kulikuwa giza sana kwa majuma mbili. Wakati tulitoshwa, ndugu na dada wenye upendo walituambia kama kuhuzuria mikutano kwa ajili ya ile masomo haimaanishe kuwa tunavunja musimamo wetu wa kutounga mukono upande wowote. Tofauti na ile, tulipaswa kuona ile kuwa nafasi ya kutoa ushahidi muzuri. Wale ndugu wenye upendo walitusaidia kuwa na hekima na usawaziko zaidi wakati tuko nakamata maamuzi.

 Juu walinizoeza kwa uvumilivu, niliona kama Yehova ananipenda na kunihangaikia. Kwa mufano, mufungwa moya mwenye alikuwa padiri alichaguliwa ili kusimamia kazi ya kufanya hesabu. Wakati tulikuwa nakutana saa ya kula alikuwa nanisalimia kwa kusema hivi: “Jambo mutoto wa Ibilisi!” Kisha mufungwa fulani akaniambia kama na miye nimujibie mu njia yenye itafanya akwazike. Kwa hiyo nilimujibu hivi: “Jambo Baba!” Juu nilimujibu vile, nilipigwa sana. Wakati ndugu zangu walijua mambo yenye ilinifikia, walinisaidia nielewe kama nilijiendesha mubaya. (Mezali 29:11) Kwa hiyo nilimuomba padiri musamaha.

 Mbele wanipeleke mu kambi ya kazi ya nguvu, nilikuwaka nahuzuria mikutano ya Kikristo kwa siri, usiku ao asubui sana. Juu mu ile kambi hamukuwa fasi ya kujificha, kila siku miye na ndugu zangu tulikuwa nasimama pamoya fasi kwenye walinzi walikuwa natuona ili kuzungumuzia maandiko fulani yenye tulikuwa tulishaandika ku makaratasi fulani ya kidogo-kidogo. Kusudi yetu ilikuwa kuchunga maandiko mingi mu akili na tukuwe naikumbuka kwa ukawaida. Kama polisi fulani anatokea, tulikuwa nameza haraka ile makaratasi.

Juu mu kambi hamukukuwa fasi ya kujificha, Mashahidi wa Yehova walikuwa wanasomea Biblia fasi kwenye walinzi walikuwa wanawaona

Hata kama Nilikuwa mu Uhamisho Mungu Aliendelea Kunipenda

Ku mwanzo wa miaka ya 1960, kisha Georgiy kutoshwa mu kambi ya kazi ya nguvu

 Mu 1959, nilitoshwa mu kambi na nikapelekwa mu eneo ya Karaganda mu Kazakhstan. Hata kama sikukuwa huru kabisa, niliomba wenye mamlaka wanipatie siku 20 juu niende kufunga ndoa. Nilifanya safari ya kuenda Tomsk mu inchi ya Urusi. Kule, nilikutana na dada muaminifu na mwenye umbo ya muzuri mwenye kuitwa Maria. Kama kawaida yangu, sikuenda mbali. Mara moya nilimuambia hivi: “Maria, sina wakati ya kukuchumbia. Tuoane!” Maria aliitika, na tukafanya sherehe ya ndoa ya kidogo. Maria alivutiwa na miye juu alijua kama nilivumiliaka majaribu mingi. Alikuwa tayari kunisaidia niendelee kumutumikia Yehova.​—Mezali 19:14.

 Mu miaka ya 1960, hatukukuwa huru kuhubiri nyumba kwa nyumba, lakini tulikuwa nahubiria watu kila mara wakati nafasi inajitokeza. Wakati tulikuwa naalikwa fasi fulani ao wakati wa mapumuziko ya kazi, mara mingi tulikuwa naambia watu juu ya tumaini yetu ya kuishi milele ku dunia. Tulikuwa natafuta pia nafasi za kuanzisha mazungumuzo na wengine. Kwa mufano, tulikuwa natembelea nafasi kwenye kulikuwa manyumba ya kuuzisha. Na wakati tulikuta wenye ile manyumba tulikuwa tunazungumuza nao mambo ya kiroho. Ile ilifanya miye na Maria tujifunze Biblia na watu sita wenye walifikia kuwa Mashahidi wa Yehova.

 Tulikuwa nahubiri wakati yote, hata wakati ya vote. Siku moya, polisi wenye walikuwa nafanya kazi kwa siri walikuya fasi kwenye miye na wandugu fulani tulikuwa natumikia. Wakati tulikuwa mbele ya wafanyakazi wenzetu karibu 1 000, walituuliza juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawajiingizake mu politike. Musimamizi wa kazi na wafanyakazi wengine walitutetea. Waliambia polisi kama tuko wafanyakazi wenye kutegemeka na wenye bidii. Ile ilitupatia nguvu ya kufasiria musimamo wetu kwa kutaya maandiko yenye tulikuwa najua. Matokeo ilikuwa muzuri juu wafanyakazi wa ine walipendezwa na kweli ya Biblia na wakafikia kubatizwa mbele mwaka moya iishe.

 Ku mwanzo wa miaka ya 1970, watu wengi wenye kuwa na mioyo minyoofu walifikia kuwa Mashahidi mu Kazakhstan. Kwa hiyo tuliona kama ni lazima tupange mukusanyiko mukubwa wa kwanza. Sasa tulijiuliza hivi: Tutakusanyika namna gani ili wenye mamlaka wasijue? Tuliamua kufanya mukusanyiko wa siku moya, na ileile wakati tulifunga ndoa mu kijiji yenye ilikuwa karibu na muji wa Almaty. Tulifanya mambo yote mbili wakati moya, ni kusema, kufunga ndoa na kufanya mukusanyiko wa Kikristo. Kulikuwa wageni zaidi ya 300 wenye walijiunga na miye na bibi arusi! Bibi yangu na dada wengine walipamba muzuri fasi kwenye tulikusanyikia na kisha walitayarisha chakula ya butamu. Wageni walifurahia sana mafundisho ya muzuri yenye kutegemea Biblia yenye ilitolewa na ndugu mbalimbali. Ile siku njo ilikuwa mara yangu ya kwanza kutoa hotuba yenye kutegemea Biblia mbele ya watu wengi.

Kumupenda Mungu Kulitusaidia mu Majaribu

Georgiy na bibi yake Maria wako na mutoto yao mwanamuke, Lyudmila

 Bibi yangu Maria, mwenye nilipenda sana alinisaidia sana mu maisha yake yote. Alikuwa mupole na mwenye kujitiisha, na kila mara alikuwa natia Ufalme pa nafasi ya kwanza. Hata kama alikuwa na nguvu kimwili, kwa kushitukia alipatwa na ugonjwa wenye unafanyaka mifupa isikuwe nguvu, wenye unaitwa ostéoporose. Na ule ugonjwa ulimufanya abakie mu kitanda kwa miaka karibu 16. Miye na mutoto wetu mwanamuke mwenye kuitwa Lyudmila, tulimuhangaikia muzuri mupaka wakati alikufa mu 2014.

 Wakati niliona bibi yangu mupendwa Maria iko nateseka, nguvu iliniisha. Lakini, tulisoma naye Biblia na vichapo fulani vyenye kutia moyo mupaka siku yenye alikufa. Mara mingi tulikuwa nazungumuzia dunia mupya. Na wakati fulani, nilikuwa naikala pembeni yake na niko nalia bila kutosha sauti. Lakini, kila mara wakati tulikuwa nasoma habari fulani kuhusu ahadi za muzuri za Yehova, tulitulia na kupata nguvu ya kuvumilia.​—Zaburi 37:18; 41:3.

Georgiy na Lyudmila wako ku mukutano wa Kikristo

 Tangu siku yenye nilivumbulaka kama Yehova ananipenda, niliendelea kuona kama alikuwa ananisaidia na kunihangaikia. (Zaburi 34:19) Juu nilikuwa kijana mwenye hana uzoefu, Yehova alionyesha kama ananipenda kwa kutumia watu wavumilivu ili wanisaidie nifanye utu wangu ukuwe muzuri zaidi. Hata kama nilipata magumu mu kambi ya kazi ya nguvu, Yehova alionyesha kama ananipenda kupitia Neno yake. Alinipatia pia nguvu yenye nilikuwa nayo lazima juu ya kuhangaikia bibi yangu mupendwa Maria mupaka siku alikufa. Leo, naweza kusema kama kumupenda Yehova kulinisaidia mu maisha yangu yote.

a Kazakhstan, Moldova, na Ukraine zilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti mupaka mwaka wa 1991.