Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mambo ya Walawi 19:16 iko na amri yenye inasema kama ‘haupaswe kuweka katika hatari uzima wa’ mutu mwingine. Ile amri inamaanisha nini, na inaweza kutufundisha nini?

Yehova aliambia Waisraeli wakuwe watakatifu. Ili kuwasaidia wakuwe vile, aliwaambia hivi: “Haupaswe kuzunguka-zunguka ili kueneza maneno ya kuchongea kati ya watu wako. Haupaswe kuweka uzima wa mwenzako katika hatari. Mimi ni Yehova.”​—Law. 19:2, 16.

Maneno “kuweka katika hatari” inafasiria muzuri Maandiko ya Kiebrania, lakini ile inamaanisha nini? Kitabu moja ya Wayahudi inasema hivi kuhusu Walawi: “Hii sehemu ya andiko iko . . . nguvu kuelewa juu haiko mwepesi kujua mambo yenye maneno ya Kiebrania inapenda kusema yenye inamaanisha neno kwa neno ‘kusimama juu ya, kusimama karibu na, ao kusimama pembeni ya.’”

Watu fulani wenye elimu wanawaza kama, ile maneno inapatana na mustari wa 15 wenye unasema: “Haupaswe kuhukumu kwa njia yenye haiko ya haki. Haupaswe kubagua maskini ao kuonyesha upendeleo kwa matajiri. Unapaswa kumuhukumu mwenzako kwa haki.” (Law. 19:15) Kisha, amri yenye inapatikana mu mustari wa 16 haupaswe “kuweka katika hatari” mutu fulani, ingemaanisha kama Waisraeli hawangepaswa kufanya jambo fulani ya mubaya mu mambo ya sheria, mu mambo ya biashara, ao mu familia. Na Mwisraeli hangepaswa kufanya jambo fulani ya kukosa unyoofu ili kujipatia faida yeye mwenyewe. Kusema kweli, hatupaswe kufanya ile mambo yote, lakini kuko njia ingine ya muzuri zaidi ya kuelewa maneno yenye kuwa mu mustari wa 16.

Fikiria mwanzo wa mustari wa 16. Mungu aliamuru watu wake wasizunguke-zunguke ili kueneza maneno ya kuchongea. Tusisahau kama, maneno ya kuchongea ni ya mubaya sana, inapita hata porojo. Hata kama porojo nayo inaweza kuleta matatizo fulani. (Mez. 10:19; Muh. 10:12-14; 1 Ti. 5:11-15; Yak. 3:6) Mara mingi, maneno ya kuchongea inakuwaka na kusudi ya kuharibishia mutu sifa. Muchongezi anaweza hata kutoa ushahidi wa uongo juu ya mutu mwingine, hata kama ile inaweza kutia uzima wa ule mutu mu hatari. Mukumbuke wale wachongezi wenye walitoa ushahidi wa uongo juu ya Naboti, na namna ile ilifanya auawe kwa majiwe bila haki. (1 Fa. 21:8-13) Kwa hiyo, muchongezi anaweza kuweka uzima wa mwingine mu hatari, sawa vile sehemu ya pili ya Mambo ya Walawi 19:16 inaonyesha.

Zaidi ya ile, mutu fulani anaweza kuchongea mutu mwingine juu tu anamuchukia. 1 Yohana 3:15, inasema hivi: “Kila mutu mwenye anamuchukia ndugu yake ni muuaji, na munajua kama hakuna muuaji mwenye uzima wa milele unakaa ndani yake.” Tena, kisha Mungu kusema haupaswe kuweka uzima wa mwenzako katika hatari, aliongezea hivi: “Haupaswe kumuchukia ndugu yako katika moyo wako.”​—Law. 19:17.

Kwa hiyo, amri yenye kuwa mu Mambo ya Walawi 19:16 ni shauri nzito kwa Wakristo. Tunapaswa kupiganisha mawazo ya mubaya, lakini pia tabia ya kuchongea mutu mwingine. Kwa kifupi, kama ‘tunaweka katika hatari’ mutu mwingine kwa kuacha chuki ao wivu ituchochee kusema maneno ya mubaya juu yake, ile itaonyesha kama tunamuchukia. Wakristo wanapaswa kabisa kuepuka ile jambo.​—Mt. 12:36, 37.