Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Usiogope. Nitakusaidia”

“Usiogope. Nitakusaidia”

WAZIA kuwa unatembea katika barabara usiku sana. Mara moja unatambua kama mutu fulani anakufuata. Wakati unasimama, mutu huyo pia anasimama. Wakati unatembea mbio sana, naye anatembea mbio sana. Unaanza kukimbilia kwenye nyumba ya rafiki yako yenye kuwa karibu. Wakati rafiki yako anafungua mulango na kukukaribisha, unatulia kwa sababu unajua kama uko sasa mahali penye usalama.

Pengine jambo hilo halijakufikiaka. Lakini, pengine uko na mahangaiko mengine katika maisha yenye kukufanya ukuwe na uoga. Kwa mufano, unapiganisha uzaifu fulani wenye ungependa kumaliza lakini unaendelea kufanya makosa yaleyale? Umefanya siku nyingi bila kuwa na kazi na unashindwa kuipata hata kama umejikaza sana kuitafuta? Unahangaikia namna utaishi wakati utazeeka na namna utapambana na magumu ya afya wakati unaokuja? Ao kuko jambo lingine lenye linakuhangaisha?

Hata kama unapambana na magumu gani, ni jambo la lazima ukuwe na rafiki mwenye unaweza kuambia mambo yenye kukuhangaisha na mwenye kuwa tayari kukusaidia. Uko na rafiki wa sana kama huyo? Ndiyo, uko naye! Yehova ni rafiki yako wa sana, kama vile tu alikuwa rafiki wa sana wa Abrahamu, mwanaume muaminifu. Andiko la Isaya 41:8-13 linaonyesha jambo hilo. Katika mustari wa 10 na wa 13, Yehova anamuahidi kila mumoja wetu hivi: “Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja na wewe. Usitazame huku na huku, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli. Nitakushika [nitakukamata] kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa uadilifu [wa haki]. Kwa maana mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika mukono wako wa kuume, Mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.’”

“NITAKUSHIKA KWELIKWELI”

Maneno hayo ya Yehova ni yenye kutuliza sana. Fikiria kidogo jambo lenye Yehova anatuahidi kabisa. Andiko haliseme kama uko unatembea pembeni ya Yehova na kukamata mukono wake. Kama ulikuwa unatembea pembeni yake, mukono wa kuume wa Yehova ungekamata mukono wako wa kushoto. Lakini, Yehova ananyoosha ‘mukono wake wa kuume wa uadilifu’ na anakamata ‘mukono wako wa kuume,’ kama vile anakukokota ili kukutosha katika hali ngumu. Wakati Yehova anakamata mukono wako wa kuume, anakutia nguvu kwa kukuambia hivi: “Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.”

Unamuona Yehova kuwa Baba na Rafiki yako mwenye upendo? Unaamini kama atakusaidia wakati unapatwa na magumu? Yehova anakuhangaikia kabisa na anapenda kukusaidia. Wakati uko na magumu, Yehova anapenda ujisikie salama. Sababu gani? Kwa sababu anakupenda sana. Kwa kweli, yeye ni ‘musaada unaopatikana kwa utayari wakati wa taabu.’—Zaburi 46:1.

WAKATI MAKOSA YETU YA ZAMANI YANAENDELEA KUTUSUMBUA

Watu fulani wanaendelea kukumbuka makosa yao ya zamani na wanajiuliza ikiwa Mungu amewasamehe. Ikiwa unajisikia hivyo, ufikirie Ayubu, mwanaume muaminifu. Alikubali kama alifanya zambi wakati alikuwa kijana. (Ayubu 13:26) Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi, alijisikia pia hivyo na alimuomba Yehova hivi: ‘Usizikumbuke zambi za ujana wangu na maasi yangu.’ (Zaburi 25:7) Kwa sababu hatukamilike, sisi wote ‘tumefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.’—Waroma 3:23.

Maneno hayo yenye kutuliza yenye kupatikana katika Isaya sura ya 41 yaliandikwa kwa ajili ya Waisraeli. Zambi zao zilikuwa nzito sana, ndiyo sababu Yehova alisema kama angewapatia malipizi kwa kufanya wapelekwe katika utumwa huko Babiloni. (Isaya 39:6, 7) Wakati huohuo, Mungu aliwaahidi kama angekomboa wale wenye wangetubu na kumurudilia! (Isaya 41:8, 9; 49:8) Leo pia, Yehova anawaonyesha upendo na rehema wale wenye kutubu kwa moyo wote na kupenda kumufurahisha.—Zaburi 51:1.

Fikiria mufano wa Takuya, * mwenye alikuwa anajikaza ili kuachana na tabia ya mubaya ya kuangalia pornografia na kugusa-gusa viungo vyake vya uzazi ili kuamusha tamaa ya ngono. Mara nyingi, alirudilia tabia yake. Hilo lilifanya ajisikie namna gani? Anasema hivi: “Nilijisikia kabisa kuwa mutu wa bure, lakini wakati nilimukaribia Yehova katika sala na kumuomba musamaha, alinisaidia kutoka katika hali hiyo.” Namna gani Yehova alifanya hivyo? Wazee wa kutaniko la Takuya walimuambia awaite kwenye telefone kila wakati angerudilia tabia yake. Anasema hivi: “Ilikuwa vigumu kuwaita, lakini kila wakati nilifanya hivyo, nilitiwa nguvu.” Kisha, wazee walifanya mipango ili mwangalizi wa muzunguko atembelee Takuya. Mwangalizi wa muzunguko alimuambia hivi: “Sikuje hapa bila mupango. Nimekuja hapa kwa sababu wazee walipenda nikuje. Walikuchagua nikutembelee ili nikutie moyo.” Takuya anasema hivi: “Ni mimi nilikuwa ninafanya zambi, lakini Yehova alikuwa tayari kunisaidia kupitia wazee.” Mwishowe, Takuya aliachana na tabia zake za mubaya, akakuwa painia wa kawaida, na sasa anatumikia kwenye Beteli. Kama vile Mungu alimusaidia ndugu huyo, atakusaidia pia wakati unafanya makosa.

WAKATI TUNAHANGAIKA JUU YA KAZI

Watu fulani wanahangaika kwa sababu wamepoteza kazi yao na wanakosa kupata kazi ingine. Wazia magumu yenye mutu anaweza kuwa nayo wakati anatafuta kazi nafasi nyingi lakini hakubaliwe. Wakati watu fulani wanapatwa na magumu hayo, wanajisikia kuwa wa bure sana. Namna gani Yehova anaweza kukusaidia? Hawezi kukupatia kazi ya muzuri palepale, lakini anaweza kukusaidia ukumbuke maneno haya ya Daudi: ‘Nilikuwa kijana, pia nimezeeka, na bado sijamuona mutu yeyote muadilifu akiwa ameachwa kabisa, wala uzao wake ukitafuta mukate.’ (Zaburi 37:25.) Yehova anakuona kuwa wa maana sana, na anakupatia ‘mukono wake wa kuume wa uadilifu’ ili upate mambo yenye uko nayo lazima na uendelee kumutumikia.

Namna gani Yehova anaweza kukusaidia ikiwa unapoteza kazi yako?

Sara, mwenye kuishi katika inchi ya Kolombia, aliona kama Yehova alikuwa na uwezo wa kumusaidia. Alikuwa anapata feza nyingi kwa kutumika wakati mwingi katika kompanyi moja yenye kuheshimika na yenye kujulikana sana. Lakini alipenda kufanya mengi katika kazi ya Yehova, kwa hiyo aliacha kazi yake na akaanza kazi ya upainia. Hata hivyo, alikuwa anatafuta kazi yenye haingemuchukua wakati wote, lakini hakuipata. Alianzisha kazi yake ya kuuzisha kreme ya baridi, lakini feza zake ziliendelea kupunguka mupaka aliacha kazi hiyo. Anasema hivi: “Miaka tatu yenye nilifanya katika hali hiyo ilionekana kuwa mirefu sana, lakini Yehova alinisaidia nivumilie.” Alielewa ni vitu gani alikuwa navyo lazima kabisa na namna ya kuacha kuhangaika juu ya kesho. (Mathayo 6:33, 34) Mwishowe, mukubwa wake wa kazi wa zamani alimuita na kumupatia kazi ileile yenye alikuwa anafanya zamani. Sara alisema kama atakubali tu kazi ikiwa haitamuchukua wakati wote na ikiwa ataruhusiwa kuwa na wakati wa kuenda kwenye mikutano na mikusanyiko. Leo, Sara hapate feza nyingi kama vile zamani, lakini anaendelea kufanya kazi yake ya upainia. Anasema kama katika wakati huo wa magumu, alijionea mukono wa Yehova wenye upendo.

WAKATI TUNAHANGAIKA JUU YA WAKATI TUTAZEEKA

Watu wengi wanahangaika sana kwa sababu wanaanza kuzeeka na wataachishwa kazi hivi karibuni. Wanajiuliza ikiwa watakuwa na feza za kuwasaidia waendelee kuwa na maisha ya muzuri. Wanahangaika pia juu ya magumu ya afya yenye yanaweza kuwapata wakati unaokuja. Inawezekana ni Mufalme Daudi ndiye alimuomba Yehova hivi: ‘Usinitupe wakati wa uzee; wakati tu nguvu zangu zinapunguka, usiniache.’—Zaburi 71:9, 18.

Namna gani watu wenye kuzeeka wanaweza kuishi bila kuhangaika juu ya wakati unaokuja? Wanapaswa kuendelea kutia nguvu imani yao katika Mungu na kutumaini kama atawapatia kila kitu chenye wako nacho lazima. Lakini, wengine kati yao walikuwa na maisha ya muzuri sana wakati walikuwa na feza nyingi, kwa hiyo wanapaswa kujifunza namna ya kuishi maisha mepesi na kutosheka na vitu vidogo. Wanaweza hata kutambua kama kula “chakula cha mboga za majani” kuliko “ngombe-dume” inaweza kuwa muzuri zaidi kwa ajili ya afya yao! (Methali 15:17) Ikiwa unakaza akili juu ya kumutumikia Yehova, atahakikisha kama uko na kila kitu chenye uko nacho lazima wakati utazeeka.

José na Rose pamoja na Tony na Wendy

Fikiria José na Rose, wenye wamemutumikia Yehova katika utumishi wa wakati wote zaidi ya miaka 65. Katika wakati huo, walipata magumu mengi. Walihangaikia baba ya Rose, mwenye alikuwa na lazima ya musaada muchana na usiku. Pia, José alipaswa kuvumilia upasuaji wa kansere na matunzo ya kemikali (chimiothérapie). Namna gani Yehova alipatia bibi na bwana hao waaminifu mukono wake wa kuume? Alitumia ndugu mwingine na bibi yake, Tony na Wendy. Walikuwa na nyumba yenye walipenda kupatia mapainia wa kawaida bila kuwalipisha. Tony alikumbuka kama wakati alikuwa kwenye masomo ya sekondari, alikuwa anaangalia kupitia dirisha na kuona José na Rose katika mahubiri kwa ukawaida. Tony alipendezwa na bidii yao, na ilimugusa moyo sana. Kwa sababu José na Rose walikuwa wametumia maisha yao yote katika kazi ya Yehova, Tony na Wendy waliwapatia nyumba. Kwa miaka 15 yenye imepita, wamesaidia José na Rose, wenye sasa wako na miaka karibu 85. José na Rose wanaona kama Tony na Wendy ni zawadi kutoka kwa Yehova.

Yehova anakuahidi hivi: “Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.” Anakupatia pia ‘mukono wake wa kuume wa uadilifu.’ Wewe pia utamupatia mukono wako?

^ fu. 11 Majina fulani yamebadilishwa.