Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Alibarikiwa kwa Sababu ya Uvumilivu Wake

Alibarikiwa kwa Sababu ya Uvumilivu Wake

Alibarikiwa kwa Sababu ya Uvumilivu Wake

Watu wengi wenye mioyo myeupe hutaka wapendwa wao wajifunze juu ya makusudi ya Mungu na hivyo kuishi maisha yenye furaha. Huenda mtu aliyejiweka wakfu kwa Mungu alisaidiwa kufanya uamuzi huo wenye hekima kwa kuona mwenendo mzuri wa wengine, vijana kwa wazee. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa msichana aitwaye Jearim anayeishi nchini Mexico, ambaye aliwapa ndugu waliosimamia kusanyiko la siku moja la Mashahidi wa Yehova barua hii fupi:

“Ningependa kuwaeleza furaha na shangwe yangu. Miaka 18 iliyopita, kabla sijazaliwa, wazazi wangu walijifunza kweli. Mama yangu alifanya maendeleo, na baadaye mimi na ndugu yangu tukafanya maendeleo pia. Sote tulisali pamoja kwa Yehova kwamba baba yangu pia aanze kutembea katika njia ya uzima. Miaka 18 imepita na leo ni siku ya pekee sana kwetu. Baba yangu atabatizwa. Ninamshukuru Yehova kwamba hakuleta mwisho kabla ya siku hiyo ambayo tumeingojea sana. Asante Yehova!”

Bila shaka, katika miaka hiyo yote msichana huyo na watu wa familia yao walifuata kanuni zinazopatikana katika ushauri wa Mungu kwenye andiko la 1 Petro 3:1, 2, linalosema hivi: “Nyinyi wake, iweni katika ujitiisho kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa neno, wapate kuvutwa bila neno kupitia mwenendo wa wake zao, kwa sababu wamekwisha kuwa mashahidi wa kujionea mwenendo wenu ulio safi kiadili pamoja na staha yenye kina kirefu.” Na bila shaka kijana Jearim alifuata maneno haya ya Kumbukumbu la Torati 5:16: “Waheshimu baba yako na mama yako; kama BWANA, Mungu wako, alivyokuamuru.” Kufuata kanuni hizo na kumngojea Yehova kwa subira kulimletea Jearim na familia yao baraka.