Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JINSI YA KUSHINDA CHUKI

1 | Usiwe na Ubaguzi

1 | Usiwe na Ubaguzi

Biblia Inasema:

“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa [kila] mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​MATENDO 10:34, 35.

Inamaanisha Nini?

Yehova * Mungu hapimi thamani yetu kwa kutegemea taifa letu, jamii yetu, rangi ya ngozi yetu, au utamaduni wetu. Badala yake anakazia jambo la maana zaidi, yaani, jinsi tulivyo kwa ndani. Kwa kweli, “mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”​—1 Samweli 16:7.

Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:

Ingawa hatuwezi kusoma mioyo ya watu, tunaweza kujitahidi kumwiga Mungu kwa kutowabagua wengine. Jitahidi kuona sifa za mtu binafsi badala ya kufikiri ni mtu mbaya kwa sababu anatokea katika jamii fulani. Ukitambua kwamba una hisia zisizofaa kuelekea watu wengine​—labda kwa sababu ya jamii au taifa lao—​sali kwa Mungu na umwombe akusaidie kung’oa hisia hizo. (Zaburi 139:23, 24) Ukimwomba Yehova kwa unyoofu akupe nguvu za kushinda ubaguzi, uwe na uhakika kwamba atasikiliza sala yako na kukusaidia.​—1 Petro 3:12.

^ fu. 6 Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.

“Sikuwa nimewahi kamwe kuketi hivyo kwa amani pamoja na mzungu. Sasa nilikuwa mshiriki wa undugu wa kweli wa ulimwenguni pote.”​—TITUS