Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tofauti Ambayo Walimu Wanatambua

Tofauti Ambayo Walimu Wanatambua

Tofauti Ambayo Walimu Wanatambua

● Irena, mwanafunzi wa darasa la 8, anaishi huko Bulgaria katika kijiji cha Kurtovo Konare. Mama yake alimpa mwalimu wake kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi wakati wa mkutano kati ya mwalimu na mzazi.

Muda fulani baadaye, mwalimu huyo, akiwa ameshika kitabu hicho, alimwita Irena mbele ya darasa. “Leo wewe ndiye utakayefundisha darasa,” akamwambia Irena. “Nimechagua sura moja ambayo utatusomea, nami ningependa utueleze jinsi familia yenu hufuata mapendekezo yaliyoonyeshwa.” Sura aliyochagua ilikuwa na kichwa “Sababu Gani ‘Niheshimu Baba Yangu na Mama Yangu’?”

Irena alipokuwa akienda mbele ya darasa, wanafunzi fulani walisema kwamba wazazi wake walikuwa tofauti. Mwalimu aliwakatiza na kuwauliza: “Mnajua ni kwa nini familia yao ni tofauti? Ni kwa sababu wao hujifunza Biblia. Nimefundisha kaka zake [Irena], na katika muda wote ambao nimekuwa mwalimu sijawahi kuona watoto walio na heshima na waliolelewa kwa njia nzuri kama wao.”

Kisha mwalimu akamwomba Irena asome. Baada ya kusoma fungu lililoeleza kwamba Mungu aliwapa wazazi haki ya kuweka sheria, mwalimu alimwuliza: “Irena, ndivyo ilivyo katika familia yenu? Je, ninyi huona kuwa kila kitu ambacho wazazi wenu wanasema ni sheria?”

“Kila mmoja wetu ana maoni yake,” akaeleza Irena, “lakini Biblia inasema kwamba watoto wanapaswa kuwaheshimu wazazi wao na kujitiisha kwao, nasi hufanya hivyo. Hata hivyo, tunaruhusiwa kuzungumzia jambo hilo pamoja, na kila mmoja wetu anakuwa na nafasi ya kueleza maoni yake.” Darasa hilo lilipokwisha, kila mtu alikuwa ameridhika.

Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa.

Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.