Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

What Do You Know About Jehovah’s Witnesses?

What Do You Know About Jehovah’s Witnesses?

Mwanafunzi mmoja wa uandishi wa habari nchini Denmark aliandika hivi: “Nilisoma mambo mengi kuwahusu Mashahidi wa Yehova kwenye Intaneti, nikasikiliza uvumi kuwahusu, na kusikiliza maoni ya watu wenye ubaguzi. Hilo lilinifanya niwe na maoni yasiyofaa kuwahusu Mashahidi wa Yehova”

MWANDISHI huyo wa habari alihoji familia moja ya Mashahidi wa Yehova. Matokeo? “Maoni yangu kuwaelekea Mashahidi yalibadilika punde tu nilipoingia nyumbani mwao!” akaandika. “Huenda watu hawawajui vizuri, au labda sisi huwahukumu haraka. Mimi nilifanya hivyo. Na niligundua kwamba nilikuwa na maoni yasiyofaa.”—Cecilie Feyling, mwandishi wa Jydske Vestkysten.

Baada ya kufanya kazi na Mashahidi wa Yehova, mshauri mmoja wa wafanyakazi katika maduka fulani huko Ulaya alisema kwamba wao ni wafanyakazi waaminifu. Hivyo akaanza kuwaajiri Mashahidi wa Yehova.

Bila shaka, Mashahidi wa Yehova hujulikana hasa kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri. Ingawa wao hukutana na watu ambao hawapendi kuzungumza kuhusu Biblia, wengine hufurahia sana mazungumzo hayo. Watu zaidi ya milioni saba, ulimwenguni pote hujifunza Biblia kwa ukawaida pamoja na Mashahidi wa Yehova, na mwishowe baadhi ya wanafunzi hawa huwa walimu wa Biblia. Kwa mfano, nchini Marekani, Baraza la Kitaifa la Makanisa liliripoti kuwa, kati ya makanisa 25 makubwa, Mashahidi wa Yehova ni 1 kati ya makanisa 4 tu yaliyopata ongezeko.

Kwa nini mamilioni ya watu wanajifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova? Mafunzo hayo huongozwa jinsi gani? Je, wanafunzi hao wanatazamiwa kuwa Mashahidi? Hata kama hutaki kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova ni haki yako kujua ukweli. Hivyo, usisikilize uvumi kuwahusu, bali tafuta hoja za kweli. Biblia inasema hivi kwenye Methali 14:15: “Mjinga huamini kila kitu anachoambiwa, lakini mwenye busara huwa na tahadhari.”—Biblia Habari Njema.

Tunatumaini kuwa toleo hili la Amkeni! litakusaidia uwaelewe Mashahidi wa Yehova vizuri na kwa usahihi. Kwa kweli, kwa kuwa unasoma gazeti hili unaonyesha kuwa una usawaziko na uko tayari kusikiliza mambo mapya. Kwa hiyo, unaposoma habari nne zifuatazo na masanduku yaliyomo, soma katika Biblia yako mwenyewe maandiko yaliyotajwa. * Hilo ni jambo la busara na pia kama Biblia inavyosema, utakuwa ‘muungwana.’—Matendo 17:11, Union Version.

^ fu. 7 Ikiwa huna Biblia, unaweza kupata moja kutoka kwa Mashahidi wa Yehova. Ikiwa unatumia Intaneti, unaweza kusoma Biblia katika lugha mbalimbali katika Tovuti ya www.watchtower.org. (Kwa sasa, Tovuti hiyo haina Biblia katika Kiswahili). Zaidi ya hilo, Tovuti hiyo ina vitabu vingine vya Biblia katika zaidi ya lugha 380.