Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Hazina Yenye Mafundisho Yanayofaa”

“Hazina Yenye Mafundisho Yanayofaa”

“Hazina Yenye Mafundisho Yanayofaa”

● Wenzi fulani wa ndoa huko New Hampshire, Marekani waliandika hivi: “Tungependa kuwashukuru sana kwa habari nyingi mnazoandika kwa ajili yetu tunaolea watoto. Tuna binti mwenye umri wa miaka minne anayeitwa Sophia, nasi tunahisi kana kwamba tunafundishwa moja kwa moja jinsi ya kukazia kweli muhimu akilini na moyoni mwake wakati huu muhimu maishani mwake.”

Barua hiyo inaendelea kusema hivi: “Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu ni hazina yenye mafundisho yanayofaa kwa ajili ya binti yetu na kwetu pia. Picha zilizo kwenye sura ya mwisho ya kitabu hicho ndizo picha zenye kupendeza sana ambazo tumewahi kuona za Paradiso! Binti yetu mdogo hutazama picha hizo tena na tena na hilo humsaidia kujifunza kuhusu ahadi za Biblia.”

Sura ya mwisho ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, yenye kichwa “Unaweza Kuishi Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu Wenye Amani,” ina picha zenye kupendeza za ahadi za Mungu zinazopatikana katika Neno lake, Biblia.

Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho chenye kurasa 256 zinazotoshana na zile za gazeti hili. Jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa.

Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Picha inapatikana kwenye ukurasa wa 254 wa kitabu hicho